Inasemekana Hii Ndio Picha Iliyowaunganisha Diamond na Hamisa Dubai

Mwanamuziki Diamond Platnumz amerudi tena kwenye skendo na mzazi mwenzie Hamisa Mobetto baada ya habari kusambaa mtandaoni kuwa walikuwa wote nchini Dubai.

Wiki chache zilizopita Diamond alienda Nchini Uingereza, London ambako alikuwa na shoo lakini siku ya pili baada ya kufika huko Zari naye alitoka South Africa na kwenda kuungana naye London ambapo waliweka picha mtandaoni wakila bata na kufanya media tours.

download latest music    

Mapema wikiend hii mrembo Hamisa Mobetto alisafiri kutoka Tanzania kuelekea Dubai ingawa hakuweka wazi sababu ya kwenda nchini humo. Baada ya Diamond kutangaza kuwa anaenda Dubai kwa ajili ya kufanya tamasha la One festival, hapo ndipo maneno yalipoanza kuwa Diamond na Hamisa wako wote ingawa hakuna aliyekuwa ana uhakika hivyo yalibaki kuwa maneno maneno ya watu mtandaoni.

Kushoto: Diamond na Salaam SK wakiwa pamoja na mrembo huyo Kulia: Hamisa akiwa pamoja na mrembo huyo.

Leo kwenye mitandao wa kijamii kuna picha inayosambaa ikimuonyesha msichana ambaye haijajulikana kuwa ni rafiki wa karibu wa Hamisa tu au ni shabiki aliyeomba kupiga picha na Diamond na akapiga picha na Hamisa jambo lililowafanya watu wengi wahisi kuwa wawili hao walikutana na walikuwa eneo moja usiku huo.

Je unahisi Diamond na Hamisa walikuwa pamoja au ni maneno ya watu wanaotaka kuwagombanisha Diamond na Zari.

Tafadhali toa maoni yako hapo chini.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.