Irene Paul Afungukia Bifu La Zamaradi na Mobetto

Muigizaji wa Bongo movie Mrembo Irene Paul amefunguka na kupima uzito bifu lililopo kati ya rafiki yake kipenzi Zamaradi Mketema na Hamisa Mobetto.

Wiki chache zilizopita Zamaradi na Mobetto waliingia Kwenye bifu zito mara baada ya kutokea sintofahamu Kwenye mavazi ambayo Zama aliyavaa kwenye arobaini ya mtoto wake.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Irene alisema Zamaradi alipoingia kwenye ugomvi na Mobeto hivi karibuni kisa kikiwa mshono wa nguo aliyovaa kwenye arobaini ya mwanaye, yeye aliamua kujiweka pembeni kwa sababu aliogopa kuchukuliwa hatua za kisheria kwani serikali kwa sasa haitaki mchezo.

Si unajua tena siku hizi sheria za mtandao, unaweza kujifanya kimbelembele yakakukuta mazito kwa hiyo niliona nikae pembeni licha ya kwamba Zamaradi ni rafiki yangu sana kwa sababu nilifahamu pia wawili hao wangeweza kumalizana bila tatizo lolote”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.