Irene Uwoya ni Mzuri Lakini Huyo Dogo Janja Simjui- Msami

Maanamuziki wa Bongo fleva na Dansa maarufu Bongo Msami Baby amezidi kutengeneza headlines Kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuendelea  kupostiana na Ex wake Irene Uwoya.

Uwoya na Msami wameendelea kuwaacha watu midomo wazi baada ya kuendelea kupostiana Kwenye mitandao ya kijamii na kusifiana ilihali Ikiwa ni wazi kabisa kuwa Uwoya ni mke wa staa wa Bongo fleva Dogo Janja.

download latest music    

Ishu hii imeleta tafsiri tofauti kabisa hasa ukizingatia kuwa Uwoya ni mke wa mtu na hivyo kusababisha ndoa ya Uwoya na Dogo Janja kukosa heshima mbele ya Jamii.

 

Msami amefanya Interview na Enews ya EATV na kudai haoni kama ni kosa yeye kumsifia Ex wake na kumkubali kama ni mzuri kwani ni ukweli mtupu na haoni kama kamvunjia heshima:

Irene kaniposti kwa sababu anapenda ninachokifanya na ananikibali kwa nini asiseme na mimi kumuandika kama yeye mzuri kwani ni dhambi? sio dhambi kumwambia mtu yeye ni mzuri kwangu mimi binafsi naona kama ni upendo Alafu isitoshe mimi Namjua Yeye huyo mtu wake mwingine mimi simjui mimi najuana na Uwoya tu kwaiyo tuna maisha yetu na stori zetu ambazo tunaongea”.

Msami amesisitiza kuwa hawezi kuacha kuongea na Irene au kumsifia kisa tu ameolewa na haoni kama ameandika kitu kibaya.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.