Jacqueline Wolper Akiri Kuteswa Na Mapenzi

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu Jacqueline Wolper amefunguka na kutaja vitu ambavyo vinamtesa akiwa kwenye mahusiano ya kimapenzi.

Katika Interview yake na Wasafi Tv, Wolper ameweka wazi kuwa vitu viwili ambavyo ni  muda na uongo ni vitu vinavyomtesa akiwa Kwenye Mahusiano ya kimapenzi.

download latest music    

Kitu kinachonitesa na kunipa stress kwenye kwenye mahusiano ni uongo na muda. Nafanya sana kazi lakini nahitaji sana muda wa kuwa na mtu wangu, kwa hiyo uongo na muda ni tatizo sana kwenye mahusiano.

Mtu akiaanza kunidanganya au kunipa muda mchache wa kuwa naye na kuwa out of mood kabisa na ninaweza nikaamka nikamwambia it’s over bila kujali chochote”.

Lakini pia Wolper amesema uongo pekee ana kukubali Kwenye Mahusiano ni uongo mzuri:

Uongo ninaouhitaji mimi ni ule kunidanganya kuwa unanipenda, tangu nizaliwe sijawahi kuona mwanamke mzuri kama wewe, huo ndio uongo unahitajika kwa kila mwanamke”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.