Jaquar Amtolea Povu Zito Harmonize

Msanii Jaquar kutoka  Kenya ameibuka na kumtolea Povu Zito msanii wa Bongo fleva kutoka label ya WCB Harmonize Baada ya kushindwa kupiga shoo nchini humo.

Wikiendi iliyopita Harmonize alitakiwa kufanya shoo mjini El Doret nchini Kenya lakini alihairisha kufanya shoo hiyo Baada promota kushindwa kumlipa pesa waliyohaidiana.

download latest music    

Kitendo cha Harmonize kushindwa kupiga shoo kiliwauzi mashabiki wengi ikiwemo Mbunge wa jimbo la Starehe Jaquar ambaye kwenye mahojiano na Kipindi cha Mambo mseto alifunguka:

“Ni tukio la kuhuzunisha lakini mimi NAMSHTUMU sana Harmonize….wakenya wamemsupport sana, wamesupport wasanii wa nje sana. Wengine wanatumia pesa zao kupiga simu, kurequest nyimbo zao. Mimi mwenyewe siwezi nikakosa kupanda stage sababu ya balance ambayo promoter amebakisha na ni kitu nilikuwa nafanya. Kwanza nadeal na mafans wangu.

Kama Mimi ningekuwa Harmonize Saturday ningeenda kwa stage niambie watu samahani nimechelewa lakini kwa sababu mumenifikisha mahali nimefika saa hii mimi nitaperform lakini promoter hajanilipa…vitu zingine nitadeal nazo baadaye sababu bila nyinyi nisingekuwa Harmonize pale niko. Unapata kuna fans wametoka mbali hadi Eldoret kwa sababu yake. Sometimes unafaa kuanglia mafans Kwanza”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.