“Jaydee ana mapenzi ya kweli” Ray C afunguka kuhusu uhusiano wake na Lady Jay Dee

Ray C alizungumzia uhusiano wake na Lady Jaydee katika mahojiano aliyofanya hivi karibuni na Mwanaspoti. Mrembo huyo alimsifu Jaydee kwa kuwa na mapenzi ya kweli.

Ray C alisema kuwa Jaydee alimwonyesha upendo sana katika kipindi alipokuwa ameathirika na utumizi wa dawa za kulevya.

download latest music    

“Jaydee ana mapenzi ya kweli kwa msanii mwenzake. Hataki kuona anaanguka…ninampenda sana kwa moyo wake wa upendo,” Ray C alisema.

Mrembo huyo pia ushauri wake kwa matumizi ya dawa za kulevya, alisema kuwa serikali inafaa ijitahidi kutoa elimu mashuleni kuhusu athari za kutumia dawa za kulevya.

“Mie naiomba tu Serikali ijitahidi kutoa elimu mashuleni kuhusu athari za kutumia dawa za kulevya, kwani wengi wanaoathirika kwa sasa ni vijana tena wadogo na wengine ni wanafunzi na hao wanafunzi hutumia muda wa mapumziko kutumia dawa hizo hivyo kupewa elimu ni muhimu kwani hawajui athari zake wanajiingiza kama mimi nilivyojiingizaga bila kujua,” anasema.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere