JB Kuacha Kufanya Kazi Za Filamu

Msanii wa bongo movies aliyejizolea umaarufu wake nchini kutokana na kufanya kazi ya filamu kwa ufasahaa na umakini mkubwa  Jacob Steven ambae watu wengi umfananisha na mwigizaji wa filamu za kihindi anaejulikana kama  Amithabh Bhachchan amefunguka na kuongelea mpango wake wa kuacha kabisa kufanya kazi za  filamu hivi karibuni.

Katika mahojiano yake na chombo kimoja cha habari siku za nyuma JB alisikika akisema kuwa anakaribia kuacha kuigiza na hatakuwa mtu anaetokea nyuma ya kamera tu, hivyo alipokuwa anahojiwa kwa mara nyingine tena  JB alisema kuwa ni kweli kabisa kwa sasa anatarajia kucha kufanya movie lakini hii haimaanishi kuwa ataaga kabisa tasnia ya filamu nchini.

download latest music    

JB anasema kuwa kwa kuwa anauwezo wa kuongoza na kuandaa movies basi atakuwa amejikita sana katika kazi hizo mbili kwa sana, lakini filamu alizofanya bado zitaendelea kufanya vizuri sokoni hivyo bado yupo pamoja na mashabiki wake.

“Nategemea kuacha movies lakini bado sijaacha,lakini movie yangu ya mwezi ujao itakuwa ya mwisho kuigiza na ili kuwaaga mashabiki na sapotaz wangu movie hii nitaifanya kwa premire,” Alifunguka JB

Hata hivyo akifunguka zaidi kuhusu sababu ya kwanini anaamua kucha kufanya movies Jb anasema kuwa amejikuta kuwa ana mambo mengi ya kufanya hivyo anahitaji kujikita huko kwanza”Ni kweli tasnia bado inanihitaji,lakini sio kwamba hata ninaitupa, taste zangu bado zitaendelea kuwepo sana , kuhusu kwanini nimefikia uamuzi huo ni kwamba  nimejikuta nina mambo mengi sana ya kufanya, kwaiyo nimeona bora nizame huko, kwenye movies na tamthilia niwaachie na wengine” aliongezea JB

Hata hivyo akiweza bayana mambo yanayomfanya yeye kuwa busy Jb anasema kuwa “makampuni ninayofanya matangazo yana ziara zinanihitaji,nahitaji kuandaa muvi, kampuni yangu ya Jerusalem, bado kmapuni ya barazani inanihitaji pia maana nina hisa hapo, lakini pia mimi ni bosi kwenye kitengo cha masoko kwaiyo unaona jinsi gani nilivyo-busy” aliongezea zaidi.

JB  ni moja ya wasanii waliofanya vizuri sana katika movies kama Dj ben, Nakwenda kwa mwanangu, Taxi driver, Signature ambazo zilimfanya kutamba sana katika filamu.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.