Johari Awekewa Madawa ya Kulevya Baa.

Mwanadada kutoka bongo movies Johari Chagula amekutwa na janga zito baada ya kuripotiwa kuwa aliwekewa madawa ya kulevya akiwa baa ambapo alionekana akiwa hapo akama akiwa anamsubiria mtu aliepanga kuonana nae.

Akitoa habari hiyo , mtu wa karibu wa Johari Chagula amefunguka na kusema kuwa nbaada ya kuwekewa madawa ya kulevya na watu wasiojulikana , watu hao walimuibia kila kitu na kumuacha mikono mitupu.

download latest music    

Akiwa anendelea kupata kinywaji kuna watu walikuja wakakaa pembeni yake ambao hata mimi sikuwajua lakini baada ya muda johari alikwenda chooni, lakini baada ya kurudi wale wtu walikuwa hawaonekanani tena pale maeneo ya karibu huku johari akiponekana kama kusinzia hivi.

Baada ya yeye mwenyewe kuzinduka alijikuta hana kila kitu na ndipo pombe ilipomuisha na kujikuta hana kitu hata kimoja na sisis tulihisi tu kuwa amewekewa madawa ya kulevya.

Baada ya hapo GPL waliamua kumtafuta Johari ambapo  alikiri kuwa alibiwa pochi iliyokuwa na simu pamoja pesa na vitu vyake vingine vya muhimu pamoja na kwamba hakuwajua watu waliomuibia.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.