Jokate Atia Neno Maamuzi ya Diamond kwa Wanatandale.
Mwanadada jokate ambae aliwahi kuwa mtu wa karibu wa msanii diaond platinumz ambae kwa sasa ni mkuu wa wilaya ya kisarawe ametia neno lake la pongeza kwa msanii diamond platinumz kwa kuamua kurudi nyumbani alikozariwa na kutoa mkono wa shukarini kwa wananchi wa sehemu hiyo.
Jokate ambae akiwahi kuwa katika mahusiano na Diamond anasema kuwa alichofanya Diamond ni jambo la busara sana ambalo sio kila mtu angeweza kulifanya lakini yeye amefanya na Mungu aendelee kumpigania kila siku.
Jokate aliandika katika ukurasa wake wa twitter, ‘ ni jambo zuri sana kukumbuka kule ulipotoka.unabaki kuwa na mfano hai kwa vijana wengi, kile ulichokifanya leo kitadumu kwenye mioyo ya wana Tandale kwa muda mrefu sana.Ubarikiwe na uendelee kuihudumia jamii zaidi kama ulivyofanya leo. ”