Joyce Kiria Amefunguka Mazito Kuhusu Ndoa Yake

Mtangazaji maarufu wa kipindi cha ‘Wanawake Live’ cha East Africa Tv, Joyce Kiria amefunguka na kueleza mazito yanayoikabili ndoa yake na Mh. Henry Kilewo ambaye ni katibu wa Chadema Mkoa wa Kinondoni.

Joyce alitumia mtandao wa kijamii kueleza matatizo yanayomsibu ambapo alifunguka na kueleza jinsi ndoa yake ilivyomharibua maisha yake baada ya kuolewa na mwanasiasa na kupelekea kugawa mashabiki zake wa vyama tofauti na alichopo mume wake lakini pia amedai kuwa mume wake amekuwa mzigo kwenye maisha yake kwasababu yeye ndio anamuhudumia na mpaka analipa kodi ya nyumba.

download latest music    

Lakini Joyce amekiri kuwa mume wake amekuwa Ana tabia ya kumpiga kipigo ambacho kina msababishia maumivu makubwa ambapo amesisitiza hiyo haikuwa mara moja au mara mbili mume wake akainua mkono wake na kumpiga.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram amefunguka yafuatayo kuhusu changamoto na matatizo ya kwenye ndoa yake :

Yaani maisha yangu yanashuka kwa sababu yake kwa kweli sikutegemea Mimi ni mfanyabiashara, mimi ni mjasiriamali wa siku nyingi tu kwaiyo kufikia hatua ile ya kujitoa mhanga vile kumpigania mpaka kugawa mashabiki zangu siku huzi nafanya biashara zangu kwa shida sana na ndio maana nasali sana namuomba Mungu anipiganie kwa ajili yake na hili ambalo nalifanya yaani sasa hivi mimi ndio nalipa kodi ya nyumba”.

Joyce alijipatia umaarufu kwa historian yake ambapo alianza maisha kama house girl/ Mfanyakazi wa ndani mpaka kuwa mtangazaji wa kipindi maarufu cha Wanawake Live ambacho kinazungumzia changamoto mbali mbali ambazo wanawake wanakutana nazo katika maisha yao ya kila siku na amesaidia wanawake wengi sana kupata haki zao za msingi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.