Jux Amjibu Chid Benz Kuhusu Tuhuma Za Kutojua Kuimba

Msanii wa muziki wa Bongo fleva  Juma Jux amemjibu Msanii mwenzake Chid Benz ambaye siku chache zilizopita alisema wazi kuwa hadhani kama Jux anajua kuimba.

Kama utakumbuka siku za nyuma Chid Benz na Jux wameshawahi kuwa na kabifu fulani Hivi baada ya Chidi kudai kuwa Jux alimpigisha shoo kwenye Ziara ya ‘In Love and Money tour’ bila kumlipa chochote kitu.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha XXL cha Clouds Fm, Jux amefunguka haya kuhusiana na sakata hilo:

Chid Benz kusema mimi sijui kuimba sidhani kama kakosea maana huo ni mtazamo wake na sio dhambi maana ni uhuru wa kuongea, nilikosea kumwambia Chid Benz nitakucheki maana nilikutana nae kwenye Love and Money tour Dar backstage na aliomba kupanda kwenye stage na alipanda na alivyomaliza nilimshukuru na nikamwambia ‘nitakucheki’”.

Kesho na sikumcheki, kila alipokuwa akinitafuta nakuwa na mambo mengine na baada ya siku tatu nikaona anasema kwenye media nimlipe hela zake, na kiukweli ile show hatukuwa na sponsor na wasanii wote walifanya bure na kutuunga mkono, bado sijamcheki ila nitamcheki”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.