Jux Amwagia Misifa Lukuki Diamond Platnumz

Mwanamuziki wa Bongo fleva ambaye anafanya vizuri kwa hivi sasa na ngoma yake ya ‘Fimbo’ amefunguka na kumwagia sifa msanii mwenzake wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Wiki iliyopita Diamond alivunja rekodi kwa kuwa msanii wa Kwanza nchini Africa kwa kufikisha subsribers milioni moja kwenye ukurasa wake wa YouTube huku akiwafunika wasanii wakubwa kama Davido, Wizkid, Fally Ipupa na wengineo:

download latest music    

Jux amefunguka na kumwagia misifa kibao Diamond kwa mafanikio hayo aliyoyapata na kukiri kuwa ni jambo jema kwani kwa upana wake linazidi kuupeleka mbele zaidi mziki wetu wa Bongo fleva.

Jux amefunguka hayo Kwenye mahojiano aliyofanya na Dizzim Online ambapo alitiririka haya zaidi:

Hiyo ni bahati ambayo sisi Watanzania tumeipata ni kitu kizuri ni sifa pia kwetu kwa sababu kama ni msanii wa Tanzania anakuwa wa kwanza kufanya kitu kama hicho Africa lazima watu watajiuliza huko Tanzania wanafanya mziki gani ndipo wanapoangalia mziki wa Bongo fleva na pia kukutana na wasanii wengine kwa hiyo ni habari njema na sio mchezo maana sio kawaida na watu wasichukulie kawaida maana kuwapata subscribers kama hao kuwapata sio mchezo”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.