Jux Apokelewa Kama Mfalme Nchini Burundi Haijawahi Kutokea

Mwanamuziki wa Bongo fleva Juma Jux amefunguka na kudai mapokezi aliyoyapata nchini Burundi ni makubwa ambayo hakuyategemea na haijawahi kutokea kwa msanii mwingine.

Jux amefunguka na kusema amepata mapenzi mazito kutoka kwa Waburundi alipokuwepo nchini kwao wikiendi iliyopita ambapo alienda kufanya shoo yake.

download latest music    

Jux amesema kuwa licha ya Mvua kubwa kunyesha siku ya shoo yake lakini bado mashabiki zake walijitokeza kumpa sapoti na kuhudhuria shoo hiyo.

Hit maker huyo wa ‘ Uniua’ alionyesha pia kufurahishwa na mapenzi aliyokuwa anapata kutoka kwa mashabiki zake baada ya kurusha video iliyokuwa inamuomuonyesha akivalishwa shanga na  vitu vingine vya asili ya warundi vinavyoonyesha heshima fulani.

Kupitia ukurasa wake wa instagram Jux aliandika maneno haya kuwa shukuru mashabiki zake wa Burundi.

Asanteni sana Burundi sitaweza kijamii kusahau upendo wenu kwenye maisha yangu japo mvua kubwa ilinyesha lakini bado mkakubali mnyeshewe na miaka kwa wingi kabisa kwenye shoo we made history nashukuru kwa heshima yenu ya kuniimbia wimbo wa taifa kama heshima yenu kwangu ni hii haijawahi kutokea kwa msanii yoyote aliyewahi kufika Burundi… Asanteni sana”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.