Jux Atangaza Ujio Wa Albamu Yake Mpya ’The Love Album’

Staa wa muziki wa Bongo fleva Juma Jux ametangaza ujio wa albamu yake mpya itakayoitwa ‘The Love Albamu’ ambayo anategemea kuiachia hivi karibuni.

Jux ambaye kwa sasa yupo Kwenye Tour na msanii mwenzake ambaye pia ni mpenzi wake Vanessa Mdee amefunguka na kuweka wazi kuwa ingawa hajataja tarehe ya uzinduzi wa Albamu hiyo lakini ni siku za karibuni.

download latest music    

Kwenye Interview yake na Wasafi Tv, Jux ameweka wazi kuwa Albamu hiyo itakwenda kwa jina la ‘In Love’ ambayo itakuwa na nyimbo 18:

The Love album itakuwa na nyimbo 18 tarehe ya kutoka ni bado sijaitangaza lakini wayu wanaokuja kwenye shoo zetu za tour yangu na Vanessa wanapata sana Bahati ya kusikia nyimbo chache za Kwenye Albamu hiyo lakini Tour ikishaisha nitatangaza tarehe ya kutoka kwa Albamu”.

Lakini Jux alifunguka kuhusu wasanii walishirikishwa katika Albamu hiyo:

Asilimia kubwa ya nyimbo Kwenye Albamu nimefanya mwenyewe lakini wasanii ambao nimewashirikisha ni mapema sana kuwataja nadhani siku Albamu ikitangazwa rasmi basi na wasanii watatajwa”.

Jux amesema sababu ya yeye na Vanessa kufanya shoo ya pamoja ni baada ya wote kutoa albamu ambapo Vanessa ametoa Money Monday’s na Yeye anakuja na The Love Album hivyo waliiona ni wakati muafaka wa kufanya shoo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.