kajala Akanusha Tuhuma Za Kutembea Na Wanaume Za Watu

Kwa muda sasa kumekuwa na tetesi zinazomuandama msanii wa Bongo Movies Kajala Masanja , msanii mrembo mwenye mtoto mmoja wa kike na mwenye kipaji kizuri katika tasnia hiyo kuwa amekuwa akitembea na wanaume za watu na kuwapokonya marafiki zake wanaume.Kajala ameonyesha kukerwa na tuhuma hizo ambazo watu wamekuwa wakimtuhumu  na kusema kuwa ni uongo mtupu na hana tabia hiyo kabisa.Kajala anasema kuwa tuhuma hizo zinamuaribia katika kazi zake na maisha yake kwa ujumla,kwa sababu baadhi ya kiki watu wanazomtafutia hata yeye mwenyewe hazikubali.

Katika mahojianao yake na Ijumaa, msanii Kajala  amesema kuwa kwa wasanii wengine wa kike ni kawaida kutafuta kiki kupitia kufanya tabia za kuiba wanaume wa watu, lakini kwake anasema hazitaki kabisa kwa sababu ni mbaya na zinaharibu kazi zake.”kiki kama hizo sizitaki kabisa kuzisikia kwanza zinaniharibia hata hazijengi chochote  kwenye jamii yangu zaidi ya kuniletea picha tofauti  kwenye jamii yangu” anasema Kajala.

download latest music    

Hata hivyo Kajala  amekuwa akituhumiwa na tetesi za kutembea na wanaume za watu hata wale wa rafiki zake, miaka ya nyuma alituhumiwa kwa kutembea na bwana wa rafiki yake Wema Sepetu aliyejulikana kwa jina la Clemence aliyemsaidia  mpaka kutoka jela katika kesi iliyokuwa inamkabili, Kajala na Wema Sepetu walikuwa marafiki  wakubwa na walikuwa wakisaidiana katika shida mbalimbali lakini urafiki wao ulikuja kukoma bada ya kajal kutuhumiwa kutembea na mwanaume wa wema.hibvi karibuni tena kajala alikuwa katika tuhuma nyingine nzito ingawa hazikuwa na uthibitisho kuwa alikuwa anatoka na msanii Harmonize, msanii aliyekuwa mpezni wa Jackline Wolper ambae pia alikuwa rafiki wa karibu wa kajala.

Kajala ni mama wa mtoto mmoja wa kike  anaeitwa Paula ,aliezaa na mume wake wa kwanza P-Funk Majani  kabla ya kuolewa kwa mara ya pili na mwanaume mwingine ambae aliingia katika matatizo nae na kufanya waachane.Kwa sasa Kajala ni mmoja wa mabalozi wa mchezo wa bahati nasibu unaendelea kuchezwa nchi unaojulikana kwa jina la Biko.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.