Kajala Awaonya Wasanii Wanaoendekeza Bata

Muigizaji wa Bongo movie na mjasiriamali Kajala Masanja amefunguka na kuwatolea uvivu Wasanii Wenzake ambao wamekuwa wakijianika Kwenye mitandao ya kijamii wakila bata tu.

Kajala amefunguka na kusema zama za kutafuta sifa kwa kuonekana unakula sana bata zimepitwa na wakati kwani hivi sasa watu wanaangali zaidi kazi na kufanya mambo ya maendeleo.

download latest music    

Kwenye mahojiano yake Gazeti la  Risasi Jumamosi, Kajala alisema yeye kuna wakati alijisahau na kujikita kwenye mambo hayo lakini sasa ameshtuka na ndio maana hawezi kuonekana viwanja ‘akitumbua’ pesa.

Unajua huu ni wakati wa mastaa kushituka na kufanya mambo yatayowasaidia wao na familia zao siku za baadaye. Mimi nimestuka, niliyokuwa nayafanya siyo mazuri ila sasa nafanya yale ambayo mtu makini anatakiwa kuyafanya“.

Kajala ni mmoja kati ya wasanii ambao wamekuwa wakionekana busy kabisa na kupiga kazi kama mtangazaji na balozi wa Biko Tanzania.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.