Kajala Masanja Akiri Kumtembezea Bakora Mwanaye

Muigizaji wa Bongo movie na Balozi wa Biko nchini Kajala Masanja maarufu Kama ‘Kay’ amefunguka na kuweka wazi kuwa kwenye malezi ya mwanaye wa pekee Paula haoni hatari kumpa kichapo pale inapobidi.

Kajala amezaa Mtoto mmoja Paula na mtayarishaji wa muziki mkongwe nchini P Funk majani na Bongo huyo Ana umri wa miaka kumi na Sita.

download latest music    

Katika interview aliyofanya na Global Publishers, Kajala amefunguka kuhusu malezi ya Mtoto Wake huyo na kusema:

Wengine hawawezi kujua ni jinsi gani ninaishi na Paula. Unajua mimi ni mama kijana, lakini lazima mtoto wangu anitii na aishi vile ninavyotaka au ninavyomuelekeza na akinizingua ninamfundisha adabu. Lakini pia kuna wakati tunaweza kuzungumza tukacheka na kutaniana.”

Kwenye mahojiano hayo Kajala alifunguka na kuweka wazi kuwa huwa anamchapa mwanaye pale inapobidi kufanya hivyo:

Nampiga tena siyo kitoto, anaponikosea mimi ni mkali sana. Siku zote nilifundishwa na mama yangu ‘akupigaye ndiye anayekufunza’. Paula anapokosea ninamfundisha na panapostahili kumchapa nafanya hivyo japokuwa siyo mara nyingi maana Paula ni mkubwa sasa, tunakaa tunazungumza na ananielewa vizuri na kuna kipindi tunakuwa marafiki sana.”

Lakini pia Kajala alifunguka kuhusu Changamoto za kulea Mtoto Kama Single mother kwani yeye na baby daddy wake waliachana kitambo sana:

Ni magumu kwa sababu sidhani kama kuna mama anapenda kulea mtoto bila baba ila kwa sababu imenilazimu kuwa hivyo, sina jinsi na uzuri Mungu kanipa nguvu ya kusimama kama mama ingawa huwa anakwenda kwa baba yake anapopata nafasi.”

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.