Kajala Masanja Amkingia Kifua Wema

Muigizaji wa Bongo movie mrembo Kajala Masanja ameibuka na kumkingia kifua msanii mwenzake Wema Sepetu baada ya kukosolewa sana kwenye mitandao ya kijamii kutokana na kusambaza picha za utupu kwenye mitandao ya kijamii.

Kajala ameibuka na kusema kuwa huu si wakati wa kushangilia kilichomtokea msanii mwenzake ambaye pia alikuwa rafiki yake wa karibu, Wema Sepetu bali inapaswa kumpa moyo na kuwa naye karibu.

download latest music    

Kwenye interview aliyofanya na Gazeti la Ijumaa kuhusu suala la kuvuja kwa video za Wema na mpenzi wake aitwaye Patrick Christopher ‘PCK’ wakiwa faragha, Kajala alisema kuwa kila binadamu anakosea kwa sababu hawezi kuwa mkamilifu katika maisha yake yote hivyo kukosea ni jambo la kawaida hivyo anampa moyo Wema, asijione mkosefu sana na kukata tamaa ya kuendelea kufanya kitu chochote.

Sioni kama ni sawa kila mmoja kumuona Wema kama ni mkosefu kupitiliza kwa sababu najua wazi hakuna aliye mkamilifu hata kidogo na siku zote kuteleza sio kuanguka ni wakati tu wa kumpa moyo na kuwa naye karibu”.

Tangu sakata hilo litokee baadhi ya wasanii ambao walikua marafiki wa Wema wamemgeuka na kutaka afungwe ili liwe fundisho mmoja wapo ni pamoja na Steve Nyerere na wasanii wengine kama vile Ray Kigosi, Esha Buheti na wengineo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.