Karen Gadner Afungukia Ndoa Yake na Petit Man

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka katika nyumba ya vipaji Tanzania (THT) Karen Gadner amefungukia tetesi zilizomzunguka hivi sasa kwa kuwa amefunga ndoa na mdau wa muziki wa Bongo fleva Petit Man.

Tetesi za Petit kuwa na Mahusiano na Karen zilianza kupamba moto Wiki chache zilizopita baada ya kuonekana kama wanavaliana nguo lakini sakata hilo limechukua Sura mpya baada ya Tetesi za ndoa.

download latest music    

Picha zinazoonekana Kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha kama wawili hao wamefunga ndoa lakini kuna taarifa kuwa inawezekana ikawa sio ndoa bali ni video ya wimbo mpya wa Karen wanashoot.

Baada ya sintofahamu Hizi mtandao wa Bongo 5, ulimtafuta Karen na kutaka kumuhoji kuhusiana na tetesi hizo za ndoa na Petit.

Picha nilizoweka zinajielezea tayari kwa kile kilichotokea, kwa sasa siwezi kusema kitu kingine nimechoka Jamani”.

Karen alikataa kufunguka kwa undani zaidi kuhusu kilichotokea na kuwataka watu waendelee kisubiri kwani watajionea mwishoni.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.