Kitu cha Kwanza Alichoongea Rich Mavoko Baada ya Kushinda Kesi.

Baada ya kushinda kesi dhidi ya uongozi aliokuwa nao kwanza wa WCB ambapo kesi hiyo ilienda kusikilizwa katika ofizi za BASATA  nakuoneka kuwa Rich mavoko alisainishwa mkataba ulikuwa ukimkandamiza yeye pamoja na muziki wke kwa mara ya kwanza msnii huyo ametoa ujumbe mzito alkini wa kuishukuru BASATA kwa kumsaidia kutoka huko.

Katika ukurasa wake wa instagram, Rich mavoko aliandika “Nimejifunza vingi lakini kikubwa ni umhimu wa kukaa karibu na walezi wetu maana changamoto ni nyingi, na kuna mengi lakini yote mnaweza kuyajua kama tukiwa karibu na nyie, leo mmenipa maana ya neno mama ni mama hata kama akiwa kilema, hata iweje nyie ndio walezi wa sanaa yetu.”

download latest music    

Tangu kumekuwa na tetesi za Rich Mavoko kutoka katika lebel hiyo hakuwahi kuzungumza kitu chochote mpaka hapo alipomaliza kesi  hiyo na kuanza kuonekana kwa habari hiyo katika vyombo vya habari.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.