Kwa Hali Ilivyo Sasa Tanzania ni Wazi Amani Haipo sio Kama Zamani- Lady Jay Dee

Msanii Mkongwe Wa Bongo fleva Judith Wambura au maarufu kwa jina lake la usanii kama Lady Jay Dee amefunguka na kusema kwa hali ilivyo sasa Tanzania in wazi amani haipo sio Kama kipindi cha nyuma na kudai kuwa hali hiyo inaleta hofu miongoni mwa wananchi.

Lady Jay Dee aliyasema hayo katika mahojiano aliyoyafanya hivi karibuni ambapo aliulizwa nini mtazamo wake kutokana na kinachoendelea nchini aliongelea ukosefu amani hasa vitendo Kama kupigwa risasi kwa Mbunge Wa Singida Mh. Tundu Lissu na pia Meja mstaafu Wa JWTZ Vincent Mritaba kupigwa risasi na watu wasiojulikana ni wazi amani ya nchi haipo.

download latest music    

Lady Jay Alisema;

Ni kweli Tanzania hakuna amani kwa  sababu kitendo cha Mtu kupigwa risasi hadharani kinatishia amani ukizingatia kuna wasanii wengine walikuwa wanatekwa unaogopa, sehemu yenye amani vitu kama ivyo havipo, na kitendo cha Meja mstaafu Wa JWTZ  kupigwa risasi inatosha kabisa kuonyesha Tanzania Amani haipo naweza kuwa sina la kusema nikaishia kusikitika tu”.

Aidha Lady Jay Dee amesema kuwa matukio hayo yanaleta picha mbaya kwa nchi kwa kuonyesha tunakoelekea sio kuzuri, kwani nchi yetu ya Tanzania inasifika kea uwepo wake Wa Amani na Upendo na Umoja pia na mshikamano.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.