Kwanini Mahusiano Mengi Huvunjika kwa Muda Mfupi

Baadhi ya wataalamu wanaohusika na maswala ya mahusiano wanasemaukuwa sababu kubwa ya watu kuvunja mahusiano kwa muda mfupi aidha kabla ya kuingia kwenye ndoa au baada ya kuingia kwenye ndoa huweza kuwekwa katika makundi mawili , yaani kundi  la kwanza ni sababu zile zinazohusiana na mchakato wa maisha ya kila siku kabla ya kuanza kuishi pamoja na pili ni zile zinazotokana  na wawili hawa kukaa pamoja na kukutana na misuguano ya kila siku.

Sababu hizi zinaweza kuwa ni tabia za mtu binafsi anakuwa nazo kabla ya kuanza mahusiano na hataki kuziacha hivyo anaamua kuziendeleza tu,  sababu hizi huweza kuleta kutengana kwenu kwa sababu tu wawili hawa wanakuwa wamechanganya tabia binafsi za mtu mmoja mmoja na zile wanazokutana nazo katika maisha ya kukaa pamoja.

download latest music    

HASIRA KALI

kwa kawaida hakuna mtu asiekuwa na hasira, lakini hasira mbaya ni ile ambayo inakuwa ya hapo kwa hapo na kuleta madhara makubwa (short temper) , hii hufanya mtu kuwa na maamuzi ya ajabu sana yanayoweza kupelekea maumivu makali sana kwa mwenzi wake ingawa baadae anaweza kupoa na kuomba samahani lakini tayari haiwezi kuponyesha jeraha lilisababishwa na hasira yak hapo nyuma

kadri haisra na matukio haya yanapokuwa yanajirudia inaleta chuki na kupungua kwa mapenzi kwa upande mmoja mpaka kusababisha mmoja wapo kujiengua mahali hapo.

HISIA ZA MAUMIVU NA MACHUNGU.

Kuna muda mtu anakuwa na hisia za machungu muda wote na hii husababishwa sana na matatizo au maisha yeti ya nyuma kwa upande wa malezi, familia au mahusiano yetu ya nyuma,mara nyingi kuna kuwa na makumbusho ya kile kilichowahi kutokea nyuma na hii inaweza kufanya kuwa na negative reflactions ya kile kilichowahi kutokea hapo nyuma.

hali hii ufika sehmu uchosha , kama huzuni ya mwezi na hasira za mara kwa mara huendelea inaweza kufanya mtu kuchoka kuonyesha mapenzi ambayo hayarudishwi kwa hisia.

KUTOFAUTIANA KATIKA MATUMIZI YA PESA.

Fikiria kuwa kuna mtu unampenda na umeamua kumshirikisha kwa kila kitu kwa sababu tu unajua kuwa huyo ndio mwenzi wako lakini cha ajabu ni kwmaba anakuwa hana ushirikiano katika swala la pesa, hawezi kutoa pesa zake kwa matumizi yenu wawili, labda pia kipato chenu hakiwezi kufanana na kile mwenzi wako anataka kukitumia kila siku.

Anakuwa na matumizi makubwa na wala yasiyo ya lazima kila siku,  anapoulizwa  anakuwa mkali na hataki kutoa maelezo kuhusu hilo, mapenzi ya aina hii hayana muda mrefu zaidi sana yupo anayehumia sana kuliko mwingine.

Angalia mnategmea kupata pesa na mnaamua kukaa chini kupanga vipaumbele vya pesa yenu lakini cha ajabu mwenzi wako hataki kutanguliza kile cha muhimu, muda mwingine anaweza kukubali wazo lako lakini pesa inapofika mikononi mwake anafanya mambo mengine.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.