Lady Jay Dee Akiri Kumganda Spicy

Mwanadada mkongwe katika muziki Lady Jay Dee akiri kuwa kwa muda sasa tangu awe na mpenzi wake ameona kuwa ni muungano wenye kuleta mafanikio sana katika kazi zake za kimuziki ukiachana na mapenzi ambayo wamejiingiza.Mwanadada huyo amesema kuwa imekuwa ni mafanikio kwa sababu walipotoa remix ya wimbo wao wa together na mpenzi wake spicy ameona kuwa hana haja ya kutokumganda mwanaume huyo kwa sababu wanapofanya kazi pamoja zinakuwa na mafanikio zaidi.

hivi karibuni msanii huyo wa kike ametoa wimbo mwingine aliomshirikisha mpenzi wake huyo unaojulikana kwa jina la baby, na umefanya vizuri  na anaamini kuwa kuendelea kufanya kazi na spicy kutampeleka sehemu nzuri zaidi kwa sababu pia nu msanii mzuri.

download latest music    

nimeamua kumganda spicy, kwa sababu  ninaamini ni mwanamuziki mzuri na muungano wetu  huwa unafanya vizuri sana,angalia ngoma iliyopita na hii  utagundua kuwa  tunapokuwa pamoja na kufanya kazi pamoja  tunatengeneza kitu kizuri. -Alisema Jay Dee.

Lady Jay Dee yupo katika mahusiano ya kimapenzi na mpenzi wake spicy ambae pia ni msanii kutoka nchini nigeria kwa zaidi ya mwaka sasa na kuamua kufanya kazi kwa pamoja kwa sababu wote ni wasanii na wanafanya vizuri katika kazi zao.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.