Lady Jay Dee Aongelea Uhusiano Wake na Mwana FA

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo Fleva Judith Wambura maarufu kama Lady JD amefunguka kuhusiana na uhusiano mpya alionao na mwanamuziki mwenzake Mwana FA.

Lady JD na Mwana Fa waliwahi kiwa mahasimu wakubwa miaka ya nyuma kidogo lakino hivi karibuni wameweka tofauti zao pembeni na kuendelea na maisha kama marafiki.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyoyafanya na kituo cha televisheni cha East Africa Lady Jay Dee alisema anashukuru kwa kitendo cha Mwana Fa kumsapoti katika kazi take mpya aliyoitoa hivi karibuni.

“Ni jambo jema sana msanii mwenzako anapo kusapoti, na ndio kitu wasanii wengi tunapenda, sisi binadamu hivo mkae mkifahamu hakuna marefu yasiyo na ncha, nilishukuru kwamba msanii mwenzangu amenisapoti”.

Ili kuonyesha kwamba wako sawa na hawana tofauti baina yao tena Mwana Fa kupitia ukurasa wake wa Instagram aliweka kipande cha video mpya ya Lady JD unaojulikana kama ‘I miss you’  na kuhimiza watu wasikilize na kuangalia nyimbo hiyo.

Pia Lady JD aliendelea kufunguka kuwa;

“Ni wasanii ambao tulikuwa tunaelewana, na ndio maana tuliweza kufanya nyimbo nyingi ambazo ziliweza kufanya vizuri na kupendwa na mashabiki, Pia watu walikuwa wanasikitika kwa yale yaliyotokea”.

Bifu la Lady JD na Mwana Fa lilikuwa kubwa lililogawanya mashabiki ambapo waliandaa shoo siku moja lakini Jay D aliishia kujaza ukumbi na Mwana Fa aliishia kupiga ukumbi mtupu na pia kuna tetesi Jay D alimuimbia wimbo wa Yahaya Mwana Fa.

Lakini tunafurahi kuona Wasanii hawa wameamua kumaliza tofauti zao kwani wote ni wasanii wazuri sana.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.