Licha ya Kuwa Mkuu wa Wilaya,Jokate Akiri Kutoachana na Uanamitindo.

Mwanadada Jokate Mwegelo ambae hivi karibuni aliteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Kisarawe  amesema kuwa hawezi kuacha kuwa mwanamitindo kama wengi wanavyodhania kwa sababu tu yeye ameteuliwa kushika nafasi fulani katika serikali.

Jokate anasema kuwa  watu wengi wamekuwa wakijiuliza kuwa itakuwaje kuhusu kazi yake ya uanamitindo hasa baada ya kupewa cheo kingine serikalini, lakini anachoamini kuwa hiyo ni kazi yake hivyo hawezi kuacha kazi hiyo.

download latest music    

jamani mimi bado membo kwaio siwezi kuacha kufanya kazi na wabunif mbalimbali kwa sababu ya kuwa mkuu wa mkoa. na kwa sababu bado navaa, nitaendelea kuvaa nguo , vitenge, na nguo mbalimbali zinazobuniwa ila tu kwa sasa lazima kuwe na utaratibu maarum wa kuvaa lazima nibadilike kidogo.

lakini pia ikumbukwe kuwa kuna mitindo na urembo mbalimbali kama mafuta, wanja, na urembo ni lazima tuendelee nao kwa sababu tu ni maisha yetu ya kila siku.na sio kwamba nitakuwa ninashiriki sana lakini nitafanya pale kwa uweoz wangu, kwa mfano kama nguo niliyovaa sasa imebuniwa na mwanamitindo kutoka hapa nchi , sasa ntaachaje kuvaa, nitaendelea kusapoti mitindo na huu ukuu wa  wilaya wangu.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.