Linah afunguka kuhusu ndoa yake

Mwanadada mrembo ambae kwa sasa amepotea kidogo katika muziki wa Bongo Fleva kutokana na pilika pilika za uzazi mwanadada Esterlina Sanga amefunguka na kusema kuwa tutegemee ndoa siku yoyote kuanzia sasa,Linah ambaye alibamba na vibao vingi ikiwa ni pamoja na  kile cha malkia wa nguvu.

Mwanadada huyo ambae pamoja na kuwa mjamzito ,alionekana kuwa mrembo siku zote bila kuchoka na hata baada ya kujifungua amezidi kunawiri na kupendeza zaidi,lLnah kwa sasa ana mtoto mmoja wa kike   amejifungua kama mwezi tu umepita,na mtoto huyo  amepewa jina la Tracy Paris.

download latest music    

Linah amezaa na mchumba wake ambae anajulikana kwa jina la Shaban na wala hausiani kabisa katika tasnia ya muziki , amesema kuwa wapo katika harakati za ndoa ingawa baba wa mtoto huyo wana utoufati wa kiimani.

Imekuwa ni desturi kwa wanamuziki wengi wakike kujishauri sana katika swala la kubeba mimba na kuzaa huku wengine wakikataa eti wataharibu miili yao, lakini hii ni tofauti na kwa mrembo huyo Linah ambae yeye anasema kuwa alikuwa ameshaamua kwa moyo mmoja  na wala hakusita kubeba mimba kwa sababu alikuwa anatamani mtoto ivyo kubeba mimba haikumpa shida.

Akielezea kuhusu baba huyo wa mtoto ,Linah anasema kuwa “Unajua huyu mchumba wangu alinipenda tangu 2009, ndio kwanza naanza kutoka lakini hakupata muda wa kunifikia hivyo anajua kazi yangu na ndio maana niko nae amekubali kila kitu changu’

Akiongelea swala la ndoa anasema kuwa ndoa ipo karibuni, na kuhusu swala la yeye kuwa dini tofauti na baba mzazi wa mtoto wake ambae wanaimani tofauti Linah anasema kuwa yeye wala haoni shida yoyote kuolewa na mtu wa dini tofauti,

Msanii huyu wa kike ukiacha katika kupitia katika mahusiano tofauti mpaka kufika hapa alishawahi kuwa na mahusiano na msanii mwenzie kutoka THT Amini lakini waliachana, na alipoulizwa kuhusu amini linah alijibu “Mimi na Amini tunaheshimiana sana kwa kuwa tayari ana mke wake na mimi nina mtu wangu”

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.