Linah Sanga: Namiliki Studio Lakini Siwezi Kuwa Producer

Mwanamuziki wa Bongo fleva Linah Sanga ameongelea hali yake ya kimziki na kufunguka kuwa pamoja na kwamba anamiliki studio ya mziki lakini hajawahi kufikiria wala kudhani kuwa anataka kuingia studio na kuwa producer.

Linah amefunguka na kudai kuwa kwa msanii kufanya kazi ya kuimba na kuwa producer inakuwa ngumu ndio maana kuna watu wako maalumu kama mproducer na wengine wako maalumu kama wasanii. Ingawa kuna wasaniiambao wanafanya vyoye viwili nikimaanisha ni ma-producer na wakati huo huo ni wasanii kama msanii kutoka kundi la Navykenzo Nahreel ambaye mbali ya kuwa msanii kutoka kundi hilo lakini pia ni producer kutoka katika lebo yake ya The Industry ambayo inasimamia wasanii mbalimbali.

download latest music    

Linah alipofanya mahojiano na Dizzim online alifunguka yafuatayo kuhusu mziki wake na kikataa kuwa producer :

Mimi ninachoamini kwenye fani hii kama muimbaji basi imba kwa sababu huwezi kufanya kazi mbili kwa wakati mmoja, yaani ukifanya huku unaimba na huku una-produce basi lazima sehemu moja kati ya hizo mbili utajikuta unaharibu kwa sababu utajikuta mwisho wa siku unaegemea upande mmoja, kwa iyo mimi sijawahi kufikiria kuwa kama nataka kuwa producer muda wowote kuanzia sasa mimi nataka tu kubaki kuwa mwanamuziki na kuendelea kuimba na kuwaachia kazi ma-producer wenyewe”.

Linah alijifungua mtoto wake wa kwanza wa kike miezi michache iliyopita jambo lililosababisha ukimya wake kwenye muziki kwa kipindi kirefu lakini Linah amehaidi kurejea studio mapema mwakani mwezi wa kwanza.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.