Linah:Hutakiwi Kumuachia Mwanaume Wako Mwanamke Mwingine

Msanii wa muziki bongo ambae alikaa kimya kwa muda baada ya kupata ujauzito na kuingia katika majukumu ya kulea , Linah Sanga amefunguka na kuongelea swala lake yeye na baba mtoto wake kufunga ndoa kama ilivyotokea hivi karibuni kwa msanii mwenzake wa kike Shiloleh,Linah anasema kuwa watu wengi wamekuwa wakimuuliza na yeye anafunga ndoa lini lakini anachojua yeye ndoa ni mipango ya Mungu hivyo hawei kupanga kitu.

Linah anasema kuwa anapenda sana kufunga ndoa na kukaa kinyumba na mwanaume wake aliyezaa nae mtoto kwa sababu hapendi kuzaa mtoto kila mtu na baba yake labda itokee sababu ya kumfanya kuachana na baba wa mtoto wake iwe kubwa lakini sababu haiwezi kuwa ni mwanamke mwingine.

download latest music    

Siwezi kujipangia nafunga ndoa lini, kwa sababu hata shiloleha hakuna aliyejua ataolewa lini .lakini kama mwanamke napenda kuolewa na ninapenda kuolewa na baba wa mtoto wangu kwa sababu katika maisha yangu nilisha apa sitatka kuzaa zaa nje huko  na baba tofauti tofauti napenda watoto wangu wawe na baba huyohuyo na mimi mama yao.

yaan labda kuwe na sababu kubwa sana ya kunifanya niachane nae na watu waone kabisa hapa linah alikuwa anafaa kuachana na huyu kuzaa na mtu mwingine.lakini so far utakiwi kumuacha mwanaume wako uanempenda kwa sababu ya mwanamke mwingine yoyote, yaani hiyo sio reason kubwa sana.unless na wewe uwe na mambo yako mengine  lakini huwezi kumuacha mwanamke wa malengo yako.

Akiongelea kuhusu kurudi katika muziki Linah anasema kuwa  kwa sasa anaanza kujipang kurudi katika muziki  kwa sababu ameshamaliza kulea na atakuja vizuri.akiongelea kuhusu tamko la kuvaa uchi linah anasema kuwa  inabidi ifafanuliwe kuvaa uchi kukoje kwa sababu kuna nguo unavaa zinakuwa za kawaida tu lakini inaweza kutasfiriwa kuwa ni nguo za uchi.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.