Lulu Ana Baba Wengi ;-Mama Kanumba

Mama wa msanii  Kanumba amefunguka na kusema kuwa hana chuki na msanii Lulu Michael na hata kama itatokea mwanadada huyo akamwalika katika ndoa yake inayonuka sasa hivi katika mitandao ya kijamii wala hatosita kwenda ingawa anachofahamu yeye ni kuwa lulu amekuwa na baba wengi sana.

Mama Kanumba anasema kuwa endapo familia itamuona kama yeye ni moja ya watu wenye sifa za kwenda katika harusi hiyo basi itakuwa kheri kwake na wala hatokataa kupokea heshima hiyo ingawa pia anaona kuwa hana vigezo kwa sabau harusiitakuwa na baba wengi.

download latest music    

Akiongea na EATV, Mama Kanumba anasema kuwa hawezi kutoa tafsiri halisi ya maneno hayo alkini alisema ‘Unajua kanumba alikuwa na baba mmoja tu na Mungu pekee ndi wa pili  lakini lulu ana baba wengi sana na kama wote wataona kuwa nina kidhi vigezo vya kuhudhuria harusi ya binti yao nitakwenda”Hapa Duniani sina chuki na Lulu kabisa na mimi akili yangu ni moja tu kumuomba mungu maana yeye ndio anayetoa hakisawa kwa tajiri na hata masikini pia.

Mama huyo amekuwa akiongea maneno tofauti kila kukicha kwa sababu mara nyingi amekuwa akionekana ana kinyongo na Lulu hasa kutokana na hukumu aliyowahi kupewa mwanadada huyo baada ya kumuua Kanumba bila kukusudia.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.