Lulu DIva na Rich Mavoko Waendelea Kuficha Penzi Lao

Msanii wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB Rich Mavoko na msanii mwenzake Lulu Diva wamedaiwa kuendelea kuficha penzi lao.

Kwa muda mrefu imekuwa ikisemekana kuwa Lulu DIva na Rich Mavoko ni wapenzi na hata tetesi hizo zimesapotiwa na picha zao mbali mbali ambazo zimekuwa zikionekana wakiwa pamoja.

download latest music    

Tetesi za wawili hawa kuwa pamoja zilianza tangu mwaka jana baada ya kudaiwa Lulu Diva ametoswa na mpenzi wake na hata mahari yake aliyotolewa kirudishwa baada ya kudaiwa kuchepuka na Mavoko.

Baada ya kutoa wimbo wao unaoitwa Ona unaofanya vizuri kwa hivi sasa wawili hao wamedai kuwa ukaribu wao ulikuwa kwa ajili ya kazi tu lakini hawana mahusiano yoyote zaidi ya urafiki wa kawaida.

Kwenye mahojiano na Mikito Nusunusu, Lulu Diva alisema kwamba, tetesi hizo si za kweli na zilitokana na watu kuunga baadhi ya video na picha na kuonesha kwamba wapo kwenye mahaba lakini si kweli, yupo karibu na jamaa huyo kwa sababu za kikazi.

Mimi na Rich hatujawahi kuwa na uhusiano wowote, ni mtu wangu, tunasaidiana kwenye kazi, maana ndiye kanitungia hata wimbo wangu mpya wa Ona, kuhusu mapenzi hapana kiukweli”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.