Lynn Akiri Kuvutiwa na Rayvanny na Dogo Janja

Video vixen na msanii wa Bongo fleva Irene Godfrey Louis maarufu kama Lynn ameibuka na kuweka wazi kuwa wasanii waliomvutia kwenye Sanaa ni Mastaa wa Bongo fleva Rayvanny na Dogo Janja.

Wiki mbili ziizopita Lynn aliingia rasmi kwenye tasnia ya Bongo Fleva kwa kutambulisha wimbo Wake Mpya ‘Chafu’.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Jumamosi, Lynn alisema kwa kipindi kirefu alikuwa na nia ila alikosa mtu wa kumshauri, lakini baada ya kuwasikilizisha nyimbo zake, Rayvanny na Dogo Janja walimtia moyo kuwa anaweza.

Muziki ni moja ya malengo yaliyokuwa ndani yangu, lakini ndoto zangu niliona kama zinakufa kutokana na baadhi ya watu kunikatisha tamaa. Lakini ilikuwa tofauti kwa Rayvanny na Dogo Janja ambao walinipa moyo kuwa naweza ndipo nikatoa wimbo wangu haraka”.

Lyyn ambaye ameachia ngoma inayokwenda kwa jina la Chafu na kusifia mapokezi kuwa ni mazuri kuliko alivyotegemea hivyo amepanga kuachia mwingine fasta.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.