Lynn na Tunda Vitani Kisa Penzi La Diamond

Video vixen aliyejizolea umaarufu Kupitia video ya wimbo wa Rayvanny ‘Kwetu’ Lynn ameingia Kwenye vita kali na video queen mwenzake Tunda Sebastian na inadaiwa kisa ni Diamond.

Global Publishers wanaripoti kuwa warembo hao hivi sasa ni kama Paka na panya kutokana na wote wawili kumpenda Diamond na kuchanganywa kwa wakati mmoja.

download latest music    

Kwa mujibu wa chanzo cha GPL, mrembo Lynn ambaye haambiliki kwa Diamond, mara baada ya kusambaa kwa video ya Tunda na Diamond pamoja  ndipo lilipotangazwa bifu jipya mjini kati ya Tunda na Lynn.

Si unajua ni juzi tu Lynn alidaiwa kuzawadiwa mpaka gari na Chibu (Diamond) wakati wa bethidei yake?

Sasa hiyo video ya Tunda imemtibua Lynn na timu yake kwa sababu Lynn humwambii kitu kwa Diamond ‘so’ sasa hivi ni mwendo wa vijembe tu huko social media (mitandao ya kijamii).

Wenyewe wanasema kama mwanamke akitaka kumtibua Lynn, basi ajisogeze kwa Diamond kama alivyofanya Tunda maana ameshasema kuwa yupo tayari kuolewa na jamaa huyo, sasa hataki mtu amtibulie”.

Baada ya Tetesi hizo za bifu gazeti hil lilimsaka Tunda ili kumhoji kuhusu bifu na Lynn ambaye alifunguka:

Jamani kama ujuavyo ile ilikuwa ni sherehe na kila mtu pale alikuwa ameshakunywa (amelewa) na wengi walikuwa wanacheza, nashangaa sana wameniona mimi tu ndiye nilikuwa nacheza na Diamond, kama siyo mambo ya ajabu ni nini?.

Mimi kucheza na Diamond imekuwa ishu kubwa, kitu ambacho kinanishangaza sana. “Ina maana watu waliniona mimi tu? Lakini mimi naona ni kitu cha kawaida kabisa kwangu hivyo watu wasipate tabu sana,” alisema Tunda. Alipoulizwa kuhusu mwanaume wake anasemaje juu ya video hiyo, Tunda alisema kuwa, kwa sasa hana mtu anayemhofia kwani alishaachana na Casto Dickson muda mrefu.”.

Lynn alipotafutwa ili kujibu tuhuma hizi alikataa kuzungumza chochote Lakini tangu sakata hili litokee Diamond ameonekana kwenye party mbili tofauti akiwa na video vixen mwingine maarufu kama Kim Nana.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.