Mabeste Afungukia Bifu Lake na Juma Jux

Msanii wa muziki wa Bongo fleva ambaye anafanya muziki wa kurap Venance Mabeste maarufu kama Mabeste aliyewahi kuhit na ngoma zake kama ‘Sirudi nyuma’ na ‘Baadaye sana’ amefungukia bifu lake na msanii mwenzake Juma Khalid ‘Jux’.

Mabeste ambaye aliwahi kuhit sana miaka kama nane iliyopita ameachia ngoma mpya, ngoma inaitwa Chakusema ambayo imefanywa na Prodyuza Rush The Don huku kichupa kikifanywa na Paxpyne.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Mabeste amefunguka kuhusu mengi lakini moja kati ya vitu vilivyokiki siku za nyuma kidogo ni bifu lake na Jux na anafunguka zaidi:

Kuna hali ya kutoelewana tu ilitokea huko nyuma na sipendi kuizungumzia sana. Lakini Jux ni mshikaji, tumetoka mbali sana kabla hata hajaenda China kwa ajili ya masomo”.

Lakini pia Mabeste amefunguka kuhusu uhusiano wake na ushkaji wake na Jux kwa sasa unaendaje:

Siyo mbaya. Ninamshukuru, ingawa hatukutani kama ambavyo ilikuwa zamani. Kwa sasa tumekwishakuwa watu wazima, kila mmoja ana majukumu yake, kwa hiyo muda mrefu huwa unapita bila kukutana wala kuwasiliana“.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.