Madee Ajibu Kashfa Za Dudubaya Kuhusu Muziki Wake

Ikumbukwe kwamba kipindi cha nyuma kidogo katika kipindi cha Friday Nite Live kinachorushwa na East Africa Television , msanii mkongwe wa muziki nchini  Dudu Baya aliongelea baadhi ya nyimbo za wasanii nchini , na katika nyimbo izo  alipata nafasi ya kuongelea wimbo mpya wa msanii Madee aliomshirikisha msanii kutoka Nigeria Tekno unaojulikana kama ‘Sikila’ huku video ikiwa katika mfumo wa vikatuni(amination) wakimtumia Jackline Wolpre kama Video queen.

Dudubaya ambae alionekana kuipondea kidogo video iyo na kusema kwamba video ilikuwa mbaya, hata audio ilikuwa mbaya, jinsi alivyopangilia mashairi na jinsi alivyoyawakilisha pia ilikuwa ni vibaya na kumwambia kuwa hata muziki wenyewe ameiga kwa sababu wimbo ulikuwa na maadhi ya kinigeria na sio ya kitanzania, hivyo Dudu Baya alisema kuwa wimbo ule wa ‘Sikila’ haupo kama vile ambavyo yeye amemzoea made katika kufanya kazi zake.

download latest music    

Hivi karibuni Madee ametoa ngoma mpya aliomshirikisha mwanadada Nandy, na unafanya vizuri unaoitwa  ‘Sema’. Akijibu tuhuma hizo Madee alisema kuwa labda kwa kuwa yeye ni msanii mkubwa ndio maana maneno hayo yameweza kusikika sana katika mitandao”unajua labda kwa sababu Dudu Baya ni msanii mkubwa, lakini hayo ni maneneo yanayozungumzwa na kila mtu kwamba huwezi kutoa wimbo alafu watu wote wakausifia,au wakasema ndio au wote wakasema mbaya,lazima kuna watu wa ‘yes’ or ‘no’, kwaiyo Dudu Baya nae ni moja kati ya watu wa ‘no’ kwaiyo sio kitu kibaya,na pia ni ruksa kumpa mtu nafasi kusema maono yake hata mimi  ningeweza kusema nyimbo ya flani ni mbaya , kwaio kwangu ni kawaida tu, hivyo ndo vitu tunavyotamani kuvipokea kila siku ili tuwe wakubwa , changamoto zinapotufika ndio tunaongeza vitu zaidi’ alifunguka Madee

Madee aliendelea kusema kuwa yeye hajali sana pale watu wanapomuongelea maana hiyo ni moja kati ya vitu wanavyokumbana navyo wasanii” mimi napenda kuongelewa sana, ndo aana hata wewe umenitafuta baada ya kusikia nimeongelewa, hicho kwangu ni kitu kizuri” aliongezea. Imekuwa kama desturi kwa baadhi ya wasanii kusema nyimbo za wasanii wenzao, lakini kwa msanii kama Dudu Baya ambae ni msanii mkongwe yeye atakuwa ameona mengi.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.