Madee Amefungukia Tuhuma za Babu Tale Kuitelekeza Tip Top Baada ya Kuhamia WCB

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva Madee Ali amefunguka na kutoa mtazamo wake juu ya taarifa ambazo zimekuwa zikienea kwamba Babu Tale ameitelekeza Tip Top Connection na kuhamia WCB.

Tangu zamani Babu Tale alijulikana zaidi kwa kuwa meneja wa wasanii wa kundi la Tip Top Connection lililoundwa na wasanii kama Madee, Tundaman, Kassim Mganga, Keisha na wengineo.

download latest music    

Lakini baadae alianza kumsimamia staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz na label nzima ya WCB na kuanzia hapo akaanza kutuhumiwa kwa kuitelekeza Tip Top baada ya kuona anapata mafanikio zaidi WCB.

Madee amefunguka juu ya hilo alipokuwa anafanya mahojiano na Sam Misago na kudai sio kweli hajawatekeleza kwani bado wanafanya naye kazi:

Babu Tale bado tunafanya naye kazi Tip Top Connection na bado anaangalia kila kinachotokea Tip Top na hapo hapo bado Babu Tale ni meneja wa WCB”.

Madee amekiri kuwa maneno maneno yanayosemwa mtaani hayana ukweli wowote watu wanazusha hayo kwa sababu wanataka kusikia kuwa wana ugomvi lakini hakuna bifu wala hakuna tatizo kazi inaendelea kama kawaida.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.