Majibu ya UKIMWI ya Mbasha Yamtia Wazimu.

UPIMA Ukimwi siyo jambo la mchezomchezo! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya mwimbaji wa nyimbo za Injili Bongo, Emmanuel Mbasha kupagawa baada ya kupewa majibu ya kipimo hicho.

Chanzo ambacho ni mtu wa karibu wa Mbasha kilieleza kwamba mwanamuziki huyo alikwenda kupima Virusi Vya Ukimwi (VVU) na alipopatiwa majibu alijikuta akirukaruka kama yuko jukwaani akiimba nyimbo zake.

download latest music    

Mbasha, baada ya kupata majibu kwamba ni mzima, hanamaambukizi ya Virusi Vya Ukimwi alipagawa yaani kama mtu ambaye alikuwa aamini, hapo ndiyo utajua kila mtu duniani anaogopa Ukimwi iwe mtumishi wa Mungu au mtu wa kawaida,” kilieleza chanzo hicho.Risasi Mchanganyiko lilimtafuta Mbasha ambaye alikiri kupima ngoma na kujikuta akipagawa kwa furaha kutokana na kukutwa hana maambukizi.

Hata hivyo mbasha alikuja kuulizwa ni kitu gani kilimfanya achanganyikiwe alipopata majibu yake ndipo alipojibu kuwa UKIMWI hauambukizwi kwa ngono pekee hivyo unapokutwa mzima ni jambo la kushukuru Mungu.

“Nilijikuta ninapagawa kwa sababu ya ile furaha ya kukutwa mzima wa afya na siyo kwamba nilikuwa sijiamini, unajua ukimwi hauambukizwi kwa ngono tu unaweza kupata kwa njia mbalimbali kwa hiyo hapa nina furaha ya ajabu,” alisema Mbasha

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.