Mama Ashura Azidisha Mashambulizi Dhidi Ya Ali Kiba

Mchekeshaji kutoka Timamu Tv anayejulikana kama Mama Ashura ameibuka tena na kuzidisha mashambulizi yake dhidi ya msanii mkongwe wa Bongo fleva Ali Kiba.

Mama Ashura amekuwa na desturi ya kumkosoa Alikiba tangu alipoweka wazi hisia zake kuwa yeye anaamini Diamond ni msanii mkubwa kuliko Alikiba. Siku ya jumapili na jumatatu alitumia kumkosoa Alikiba kwa performance yake aliyofanya Fiesta na kudai kuwa sio mburudishaji mzuri na wala hajui kuimba live.

download latest music    

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mama Ashura ameendelea kufunguka haya kuhusiana na Ali Kiba:

 Unajua uimbaji wa muziki sio ufundi tu wa sauti, maana kuna wanaodhani kwa sababu wana ufundi wa sauti basi mziki wa Bongo wameshauwini. Big NOO yambua jinsi ya kucheza na sauti yako na linganisha na mahitaji ya muziki wako, napendaga kumtolea mfano Mondi sio kwamba pekee anayeweza au anafanya vizuri Laah ila ni mmoja wapo kati ya mfano wa kuigwa. Kipindi anatoka watu wakasema ooh hawezi kuimba anaunga unga vocal zake hazina ufundi, lakini sahivi ule muono umebadilika baada ya watu wa kimataifa kuona uwezo wake wa kucheza na sauti yake ambayo ilisemwa ni ya kuunga unga kiujanja ujanja. Wapo wengi wenye sauti nzuri na wanajua kucheza nazo mfano mwingine ni Barnaba na wengine. Sasa wale wakali wa saute wanavyo jikakamua kuimba ‘halelujah’ kwa kutumia ufundi wao wa halo ya juu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.