Mama Diamond Afungukia Uhusiano Wa Ommy Dimpoz na Zari

Mama mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi. Sandra Kassim maarufu kama Mama Diamond amefunguka na kuongelea uhusiano na kinachoendelea kati ya Zari na Ommy Dimpoz.

Siku chache zilizopita msanii wa Bongo fleva Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ na mzazi mwenzake na Diamond Zari the Bosslady walitengeneza headlines baada ya picha zao wakiwa pamoja nchini South Africa kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

download latest music    

Kwenye mahojiano na gazeti la Risasi Jumamosi, Mama Diamond amesema kuwa ukaribu wa Zari na Dimpoz ni wa kawaida kama watu wengine na kuwataka watu waache maneno maneno yasiyo na msingi.

Kwani kuna ubaya gani? Hivyo ni vitu vya kawaida kwa mtu kukumbatiana na mtu aliyekutana naye Mimi sijaona hiyo picha ambayo kamshika pajani lakini bado nasema hayo ni mambo ya kawaida tu. Ina maana Zari asiongee na watu? Watu wanasema Nasibu na Ommy wana ugomvi, mimi sijaona wakipigana, najua wanaongea na wala mimi sina ugomvi na mtu”.

Siku za nyuma Diamond aliwahi kuingia kwenye ugomvi mzito na Ommy Dimpoz uliopelekea kutukanana matusi ya nguoni hadi Ommy kumkashifu Mama Dimoand lakini tangu alipougua kuna tetesi kuwa bifu hilo limeisha na wasanii hao wamesahameana.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.