Mama Kanumba Afungukia Ndoa Ya Lulu na Majizzo

Mama mzazi wa aliyekuwa Msanii wa Bongo movie Steven Kanumba, Florah Mtegoa maarufu kama Mama Kanumba amefunguka na kusema yuko tayari kuhudhuria harusi Lulu endapo ataalikwa.

Mama Kanumba ambaye aliweka wazi chuki yake dhidi ya Lulu baada ya kukutwa na hatia ya kumuua bila kukusudia Marehemu Steven Kanumba ambapo alihukumiwa miaka miwili jela.

download latest music    

Mama Kanumba alifurahi baada ya kifungo cha Lulu lakini hivi sasa baada ya Lulu kuachiwa huru Mama Kanumba anafunguka na kusema wazi wazi kuwa hana chuki na Lulu na endapo ataalikwa Kwenye Harusi basi hatasita Kuhudhuria kwani hana kinyongo na Mrembo huyo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo cha televisheni cha East Africa, Mama Kanumba alifunguka haya:

Hapa duniani sina chuki kabisa na Lulu na mimi akili yangu kwa hivi sasa akili yangu imeegemea upande mmoja tu nao ni kumuomba Mungu tu maana yeye ndio anatoa haki sawa kwa tajiri na hata masikini pia”.

Lulu alivalishwa pete na mpenzi wake ambaye ni CEO wa EFM Majizzo ambapo ndoa yake inatarajiwa kufanyika Miezi ya mbeleni.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.