Mama Kanumba: Nilikuwa Naumia Nikimuona Lulu Anakula Raha, Nimefurahi Alivyofungwa Sahivi Zamu Ya Familia Yake Kulia

Mzazi wa marehemu Kanumba, Mama Kanumba amefunguka kuhusu furaha aliyokuwa nayo baada ya muuaji wa mtoto wake muigizaji Lulu Michael kuwekwa ndani kwa miaka miwili.

Tangu hukumu ya Lulu mengi yamesemwa huku watu wakigawanyika na misimamo kutofautiana kwani kuna watu wanasema kuwa afadhali Lulu amefungwa na kuna wanaosikitika Lulu kufungwa kwa sababu ni binti mdogo.

download latest music    

Baada ya kifo cha Kanumba, Lulu alikuwa karibu sana na Mama Kanumba lakini baadae ghafla ule ukaribu ukaisha na kusababisha tetesi kuenea kuwa wawili hao wamegombana huku sababu ikiwa haijulikani.

Kwenye mahojiano ambayo Mama Kanumba alifanya na Global TV alifunguka yafuatayo:

Kwa kweli tunashukuru haki imetendeka kwaiyo kama familia ya Lulu wamelia mimi ninalia kila siku wao miaka miwili tu atatoka mimi mtoto wangu sitamuona tena yaani harudi tena, Baada ya hukumu kutolewa tulienda makaburini kufanya misa lakini mimi sherehe yangu nitaenda kuifanya kanisani kwa kutoa shukrani ya pekee. Kwa muda mrefu familia yetu imekuwa ikiumia tukimuona Lulu nakula raha anaenjoy anafurahia iiltuumiza sana kwa muda mrefu ni bora mtu usimuone lakini anaposti anavyokula raha kweli tulikuwa tunahuzunika sana, lakini kesi ilivyoanza tulitegemea kesi haki itatendeka na tunashukuru Mungu ametutendea kwa kweli”.

Mara ya kwanza hukumu ilivyotolewa hakimu wa Lulu, Peter Kibatala aliweka wazi nia yao ya kukata rufaa lakini habari zimeenea kuwa kutokea jela Lulu amekataa kukata rufaa badala yake ameamua kutumikia kifungo chake chote cha miaka miwili.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.