Mama Mobetto Afungukia Penzi Jipya la Hamisa

Mama Mzazi wa mwanamitindo na msanii wa Bongo fleva Hamisa Mobetto, Shufaa Rutiginga maarufu Kama Mama Mobetto amefungukia madai yaliyosambaa kwenye mitandao kumuhusu mwanaye Hamisa.

Mama Mobetto amefungukia madai kuwa mwanaye Hamisa Ana mwanaume mpya ambaye siyo Raia wa Tanzania na kusema kuwa, yeye kama mama hana taarifa ya kuwa mtoto wake huyo ana mwanaume mwingine kama inavyoelezwa mitandaoni.

download latest music    

Katika mahojiano yake na gazeti la Ijumaa Wikienda, Mama Mobetto ambaye ilidaiwa kuwa aliwahi kumweka mwanaume huyo kwenye ‘profile’ yake na kuandika kuwa anampenda mkwe wake huyo, alikana madai hayo. Alisema siku zote huwezi kuwazuia binadamu wakiamua kusema mambo yao hivyo naye hajali maneno ya watu.

Mimi kwa kweli sijawahi kumweka huyo mtu, lakini pia unajua kila kukicha kwenye mitandao ya kijamii kila mtu anaongea lake. Kwa hiyo kama mtu huwaelewi, unaweza kupata tabu sana”.

Mambo ya mkwe yametoka wapi tena? Ninachojua sasa hivi Hamisa anapiga kazi tu na si vitu vinginevyo. Kwa sasa sihitaji mkwe wala sina maana siku akiwepo kila mtu atamjua tu, sidhani kama hiyo itakuwa ni siri”.

Tangu Hamisa aachane na Baba watoto wake Diamond Platnumz mapema mwaka huu amesema Hana mpango wa kujiingiza kwenye Mapenzi kwa sasa Bali anataka apige kazi ili aweze kuwalea watoto wake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.