Mange Kimambi Amtolea Povu Zito Wema Baada Ya Kutangaza Kurudi CCM

Mwanaharakati wa siasa mtandaoni Mange Kimambi amemtolea povu zito muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu baada ya kutangaza kuwa anahama Chadema na kurudi kwenye chama chake cha zamani CCM.

Habari zilianza kusambaa tangu mwanzoni mwa wiki hii kuwa Wema anampango wa kurudi CCM. Leo kupitia ukirasa wake wa Instagram Wema ameujulisha uma wa watanzania kuwa ameamua kuondoka Chadema na kurudi chama chake cha zamani CCM Wema alifunguka kama ifuatavyo:

download latest music    

Siwezi kuendelea kuishi kwenye nyumba inayonikosesha amani, Peace of mind is everything for me natangaza rasmi kuondoka Chadema na kurudi Nyumbani there is no place like home….feels good to be back”.

Baada ya kutoa tangazo hilo la kuamua kurudi CCM Mange hakupoteza muda kutoa maoni yake juu ya kitendo alichofanya Wema, kupitia ukurasa wake wa Instagram Mange alimwagia Wema povu hili:

Not sure what to say i only blame her for not being strong enough Nyerere alikaa jela for 27 years she could have taken 2 or 3 years ya hiyo kesi yake Kimara nzima imebomolewa nyumba na wanaishi sembuse yeye mwenye kubwa. Na lipshone zako walizozipiga marufuku so what?  Ungekomaa na msimamo wako serikali ingechoka kukuandama Wema your weak very weak! Hujawaangusha Watanzania tu umejiangusha wewe mwenyewe, your fans na Watu wote who cared for you”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.