Mange Kimambi: Diamond Kaweka Rekodi Feki

Mange Kimambi ameibuka upya na kudai kuwa rekodi ambayo Diamond Platnumz ameweka ni feki Hili limekuja baada ya Diamond kuachia wimbo wake mpya siku mbili zilizopita uitwao Hallelujah aliomshirikisha  mwanamuziki Morgan Heritage, wimbo huo ulifanikiwa kufikisha jumla ya views million mbili kwenye mtandao wa Youtube ndani ya siku moja.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mange alifunguka yafuatayo juu ya suala hilo;

download latest music    

“#IssaFakeRecord Amenunua viewers huo ndo ukweli!!! Samahani kwa ntakaowakwaza…. Baba Dully ajifunze kukubali na kushindwa sometimes, hakuwa na haja ya kununua viewers ili tu avunje rekodi ya Ali Kiba”.

Mange aliendelea kusimamia msimamo wake juu ya suala hilo japokuwa alipokea ushindani mkubwa shidi ya mashabiki wa Diamond ambao walimlaani vikali;

“Mtanitukana sana Team Diamond ila wote mnajua kuwa sisemagi uwongo na maneno yangu kwa njia moja au nyingine huwa lazima mwisho wa siku yawe ya kweli! Naamini soon mtakuja kujua kuwa Mange aliwaambia ukweli kuwa Diamond alinunua viewers! Leo mtanichamba ila siku moja ukweli utajulikana. Haiwezekani nyimbo imetrend namba moja Tanzania peke yake ikapata waangaliaji milioni moja ndani ya masaa kum na tano wakati Seduce me iliyotrens Afrika Mashariki nzima ilipata waangaliaji milioni moj ndani ya masaa thelathini na nane, it doesnt make sense ata all #fact”.

Diamond alivunja rekodi hiyo iliyowekwa na hasimu wake Ali Kiba ambaye kwa kupitia wimbo wake wa seduce me alifikisha waangaliaji milioni 1 ndani ya masaa 38 na Diamond juzi alifikisha waangaliaji wa Video yake hiyo milioni 2 ndani ya siku moja.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.