Mange Kimambi: Jaji Ametenda Haki Lulu Kufungwa, Big Up Kwake

Mwanaharakati wa Siasa Mange Kimambi amefunguka mapema leo mara baada ya hukumu ya Lulu kutoka na kuhukumiwa miaka miwili jela, Mange amedai Lulu amestahili hukumu hiyo.

Tangu kesi hii imeanza Mange amekuwa muwazi na kusema anatamani Lulu afungwe ili tu ajifunze kidogo ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram aliandika:

download latest music    

Mimi ningekuwa hakimu ningemkuta na hatia ya kuua bila kukusudia, Ila ningempa adhabu ndogo tu ya mwaka mmoja au miaka miwili jela. Mtu kafariki wakati wa ugomvi na aliyekuwa anagombana naye alikimbia that means kuna kitu alifanya bila kukusudia kilicho sababisha  hicho kifo, anyways kila mtu na Bahati yake”.

Baada ya Jaji kutangaza hukumu yake na kusema miaka miwili Mange alifunguka kuwa anafuraha kuwa haki imetendeka na sheria imekata pande zote:

Breaking News…Lulu amekutwa na hatia ya kuua bila kukusudia na amehukumiwa miaka miwili jela..Jaji ametenda haki Big up Jaji Lumanyika umetenda haki!! Sio kama nimefurahi Lulu kufungwa ila nilichotaka kuona nihakuna double standards, nilitaka kuona haji inatendeka na Lulu anstahili hiyo miaka miwili jela labda itampa muda wa kufikiria ni kwa jinsi gani matendo yake yalivyo muumiza Mama Kanumba na famili yake labda akitoka atakuwa more humble. Lakini pia mwanasheria wa serikali achukuliwe hatua za kinidhamu afukuzwe kazi alijaribu sana kumbeba Lulu ili amsaidie kushinda kesi”.

Mara baada ya kesi hiyo kuisha Lulu alitupwa jela na Mama Kanumba aliongea na Waandishi wa Habari huku akishukuru Mungu kwa haji kutendeka lakini Mama Lulu alionekana akiondoka mahakamani huku akiwa ameshikiliwa kwa sababu ya kukosa nguvu.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.