Mange: Wote Wanaomkosoa Hamisa Kuzaa na Diamond Wanamuonea Wivu

Mchambuzi na mdau mkubwa wa Siasa mtandaoni Mange Kimambi amewajia juu wale wote wanaomsakama Hamisa Mobeto kwa kitendo cha kuvujisha picha na video za faragha wakiwa na Diamond.

Tangu sakata Diamond na Hamisa litokee watu mbalimbali wamekuwana mitazamo tofauti kuhusiana na kilichotokea huku watu wengi wameenda upande wa Diamond na kumsakama sana Hamisa na kumuita majina mabaya kwa kitendo chake cha kuzaa na Diamond huku akijua wazi kuwa yuko kwenye uhusianao na Zari.

download latest music    

Mange amekuja juu na kuwasema wotw wanaomsema vibaya na kumuona kama shujaa kwa kitendo chake cha kuhakikisha kuwa Diamond anamkubali mtoto wao hadharani.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mange aliongea yafuatayo:

“Hamisa usikae kujutia ulichokifanya, acha waongee but you did the right thing for your child hao wanaosema haujui kula na kipofu ndo magolddiger, wewe ungekuwa golddiger ungekaa kimya ule vyako kimya kimya lakini uliamua kumpigania mwanao bila kujali. Najua ulijua tangia mwanzoni kuipeleka issue public itamuuzi Diamond lakini hata baada ya vitisho alivyokupa still uliamua  kufanya ulichokifanya. Umemsaidia sana mtoto wako unajua watu hawajui watoto wa kufichwa na baba zao wanaishije? hao watoto wana kuwa messed up maisha yao yote.Anapita nje ya jumba la babake lakini hawezi ingia kwasababu siri itajulikana hata kama baba yake anawasiliana naye kwa kuficha still itamsumbua mno mtot kujiuliza why yeye anafichwa wenzie hawafichwi yeye alikosa nini. na kibaya zaidi siku baba akifa mirathi hapati kitu kwa sababu baba hajawahi kumtambulisha lakini leo hii Diamond akifa Dylan atapata mirathi sawa na Tiffah kwa hilo hongera Hamisa”.

Pia Mange amemwambia Hamisa wale wote wanaomsema kwa kuzaa na Diamond wanamuonea wivu kwasababu wanajua mtoto wake ataishi maisha mazuri bila wasiwasi na pia wanaona wivu kwasababu Hamisa tayari amezaa na mmiliki wa stesheni ya EFM Majizzo ambaye pia ni tajiri kwahiyo wanajua wazi kuwa baba wote wa watoto wake wawili ni watu wenye uwezo kifedha.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.