“Marafiki Wanamuharibu Hamisa”- Esma Platnumz

Dada wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Esma Khan ‘Esma Platnumz’ ameibuka na kudai Hamisa ni rafiki mzuri sema watu wanatajwa kama marafiki zake ndio  wamemuharibu.

Esma amefunguka hayo kwenye ukurasa wake wa Instagram ambapo aliomba mashabiki zake wamuulie maswali yoyote na yeye angejibu na moja kati ya maswali aliyoulizwa yalimuhusu Hamisa.

download latest music    

Kama utakumbuka siku za nyuma Esma alishawahi kuwa na urafiki wa karibu na Hamisa Mobetto tena inasemekana alikuwa na urafiki na familia ya Diamond kwa miaka mingi.

Lakini urafiki huo uliingia shubiri baada ya Hamisa kuzaa na Diamond na kupelekea Bifu kubwa kati ya Hamisa na Familia nzima ya Diamond iliyopelekea urafiki wa Esma na Hamisa kuisha kabisa.

Swali la Kwanza:

Umemiss nini kutoka kwa Hamisa Mobetto alikuwa rafiki Yako sana?

Esma Akajibu:

Hamisa ni rafiki mzuri ila watu wanamuharibu tu”.

Swali la Pili:

Kwa nini hupendi Hamisa aolewe na Diamond?

Esma Akajibu:

Sijawahi kusema hivyo”.

Sakata la Hamisa na Esma lilichukua sura mpya Baada ya kumrushia tuhuma za uchawi dhidi ya kaka yake Diamond.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.