Mashabiki Wamjia Juu Mama Diamond Baada ya Kutomtaja Mtoto Wa Hamisa Kama Mjukuu Wake

Mama mzazi wa msanii Diamond Platnumz Bi. Sandrah, amejikuta katika wakati mgumu baada ya mashabiki kumsema baada ya kugoma kumtambua mtoto wa Hamisa.

Miezi michache iliyopita Diamond alikiri mbele ya uma wa Watanzania kuwa alimsaliti mpenzi wake na mama wa watoto wake Zarinah Hassan na kuzaa na mchepuko wake Hamisa Mobetto. Lakini kilichowavutia watu wengi ni kuwa Diamond hakumkataa mtoto wake bali alimkubali kwa moyo mmoja.

download latest music    

Lakini tangu kipindi hicho kipite hali imekuwa tofauti na watu wengi walivyofikiria kwani Diamond hana uhusiano wowote na mtoto wake na ni miezi michache tu iliyopita Hamisa ametoka kumburuza Diamond mahakamani na kudai kuwa tangu mtoto amezaliwa hajatoa matunzo yoyote.

Pia kwa upande wa familia ya Diamond haijaonyesha ukaribu wowote na mtoto wa hamisa Kama ilivyokuwa na watoto wa Diamond na Zari. Mama Diamond amekuwa akilaumiwa na mashabiki wengi kwa kumtenga mtoto wa Hamisa kwani anaonyesha mapenzi kwa watoto wa Zari lakini sio mjukuu wake kwa Hamisa.

Siku ya leo Mama Diamond kupitia ukurasa wake wa Instagram aliwajia juu watu wote wanaomkosoa kwa kupenda kuwaposti wajukuu zake wawili tu na hata mkwe wake Zari na hili ndio lilikuwa povu lake:

Mapenzi niliyonayo kwa wanangu hawa hayana mfano. Ninapomposti mkwe wangu Zari na mwanangu Diamond sifanyi kwa ajili ya kuwaridhisha wasiotupenda…Nawaposti kwa ajili ya mapenzi makubwa kwao na wajukuu zangu Tiffah na Nillan . Imani yangu sio kumkwaza mtu  au kumkebehi bali ninawapendaga sana. Akaunti hii ni Mali yangu kwaiyo asitokee mtu wa kunipangia cha kuposti au kujifanya mama/baba ushauri maisha kuchagua sio kuchaguliwa”.

Mashabiki walimjia juu Mama Diamond na kumtuhumu kuwa anamtumua Zari ili kumrusha roho na kumuumiza Hamisa lakini pia watu wamemsema Mama Diamond kwa kuwapenda watoto wa Zari Latino kumtenga mtoto wa Hamisa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.