Mbasha Afungukia Majibu Yake Ya Ukimwi

Msanii wa nyimbo za Injili Emmanuel Mbasha amefunguka na kuanika majibu yake ya ugonjwa wa Ukimwi aliofungukia na kukiri kupima siku chache zilizopita.

Global Publishers wanaripoti kuwa mtu wa karibu wa Mbasha kilieleza kwamba mwanamuziki huyo alikwenda kupima Virusi Vya Ukimwi (VVU) na alipopatiwa majibu alijikuta akirukaruka kama yuko jukwaani akiimba nyimbo zake.

download latest music    

Mbasha, baada ya kupata majibu kwamba ni mzima, hanamaambukizi ya Virusi Vya Ukimwi alipagawa yaani kama mtu ambaye alikuwa aamini, hapo ndiyo utajua kila mtu duniani anaogopa Ukimwi iwe mtumishi wa Mungu au mtu wa kawaida”.

Katika mahojiano yake na Gazeti la Risasi, Mbasha alikiri taarifa hizo na kudai alipagawa kwa furaha baada ya kujikuta hana magonjwa hayo:

Nilijikuta ninapagawa kwa sababu ya ile furaha ya kukutwa mzima wa afya na siyo kwamba nilikuwa sijiamini, unajua ukimwi hauambukizwi kwa ngono tu unaweza kupata kwa njia mbalimbali kwa hiyo hapa nina furaha ya ajabu“.

Mbasha alianika majibu yake Kupitia ukurasa wake wa Instagram Kwenye insta story ili kuonyesha mashabiki zake kwamba yeye ni Mzima kabisa bila Shaka:

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.