Mbasha Ajitapa Kuteketeza Pesa Kwenye Vazi La Suti

Msanii wa nyimbo za injili nchini Emmanuel Mbasha amefunguka na kuweka wazi kuwa anatumia pesa nyingi kwenye kununua vazi analodai linamuweka smart la suti.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Jumamosi, Mbasha alisema kuwa yeye Mavazi yake hajawahi kuvalishwa na mtu, huwa ananunua nguo kisha anaondoka dukani tofauti na wale ambao huvalishwa na maduka mbalimbali.

download latest music    

Ni kweli nina suti nyingi na sina anayenivalisha wala ‘sponsor’, unajua mimi napenda sana kuvaa, napenda ‘usmart’ na kunukia vizuri, naamini hata jamii imenizoea hivyo. Hapa kwenye suala la kuvaa huwa natumia pesa yangu“.

Mbasha alipoulizwa kuhusu uwezekano wa kuwepo mtu ambaye anamvalisha bure kwa lengo la kumtangazia biashara Mbasha alikana kabisa:

 

Nikwambie tu uelewe kuwa mimi najivalisha kwa pesa yangu na kama sikununua dukani huwa nashonesha kwa fundi wangu maalumu ambaye huwa nampa laki tatu ananitafutia kitambaa na kunishonea, linapokuja suala la mavazi huwa sina mchezo, nateketeza fedha bila kujali”.

Lakini pia Mbasha alijitapa kutokurudia rudia nguo Lakini pia alikiri hajui thamani ya nguo zake zote:

Ukweli siwezi kuwa na hesabu ya haraka haraka ila najua kila suti nimenunua bei gani kwani mara nyingi natumia kuanzia laki moja na nusu mpaka laki tano, inategemea aina ya suti na kitambaa chake.

Kurudia nguo kwangu ni mara chache sana, kwani kama ni suti moja naweza kuivaa mara mbili tu kwa mwezi lakini siwezi kurudia zaidi ya hapo kwani ninazo nyingi“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.