Mbasha Akiri Kumkubali Wema, Amponda Mobetto

Mwanamuziki wa nyimbo za Injili Emmanuel Mbasha ameibuka na kudai Wema Sepetu ndio Tanzania Sweetheart pekeee na sio vinginevyo.

Emanuel amesema hayo baada ya kuibuka kwa mjadala mzito katika siku za hivi Karibuni baada ya mashabiki kutaka kumvua cheo cha Tanzanian Sweetheart Wema Sepetu na kumvalisha Hamisa Mobetto.

download latest music    

Katika Interview yake na Gazeti la Ijumaa, Mbasha alisema kuwa kwa upande wake, Tanzania Sweetheart kati ya warembo hao wawili, ni Wema kwani ndiye anayestahili na hilo halina hata mjadala.

Hilo jina linamfaa aliyekuwa nalo tangu zamani (Wema), kwani ndiye aliyepewa hilo jina, kwa hivyo acha tu aendelee nalo kwa sababu ndio linampendezea”.

Siku za hivi Karibuni Mbasha aliingia katika vita kali na mashabiki wa Mobetto baada ya kuweka picha yake akiwa anapaa na ungo kufuatia tuhuma za uchawi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.